HOME

Wednesday, 4 January 2017

JE UNATAKA KUJUA JINSI YA KUINSTALL OPERATING SYSTEM !

Unaweza kujitengenezea kipato wewe mtanzania kwa kujiajili katika shughuli mbalimbali,Sio lazima uajiliwe katika makampuni makubwa ama serikalini ama mahala popote bali unaweza ukabuni namna yoyote ya kutengeneza kipato na kutimiza ndoto zako, Kwako mwanafunzi unae maliza chuo sasa ama uliepo nyumbani tu una computer yako ila una shindwa utaanza vipi kujikimu kimaisha hii ni fursa yako sasa kujua jinsi ya kuandaa Operating system (OS)  na kufanya installation katika Computer yoyote.
Kuna njia mbali mbali za kuweza kuweka Operating system (OS) katika computer yako leo nitakupa Njia mbili ambazo ni rahisi Zaidi kwako.
Katika njia zote hizo ni kwajili ya Windows 7 zote pamoja na Windows 8 zote 
VIFAA VYA KUWA NAVO KABLA HUJAANZA CHOCHOTE

Kwa njia ya kwanza hakikisha una flash Drive ambayo itakulazimu uifanye kuwa bootable bila ya kufanya hivo itakuwa sio rahisi kukamilisha zoezi lako isipo kuwa kama computer yako itaweza ku boot hivo hivo,Je utaifanya vip Flash yako iweze ku boot
POWER ISO 
Power Iso ni software inayo weza kukusaidia kutengeneza flash iweze ku boot unaweza kupata software hiyo kwa kubofya hapa http://www.poweriso.com/thank-you.htm
Kabla ya kuaandaa flash yako kumbuka window 7 au 8 itakuwa katika muonekano huu




Hakikisha ina kuwa katika mfumo wa image kama picha inavo onesha hapa chini



Baada ya kufungua software ya power Iso copy mafile ya windows na paste katika uwanja wa power iso the uta save file yako as (.Iso) image utakuwa umebadilisha

 ANDAA FLASH IWEZE KU BOOT KATIKA COMPUTER

Fuata hatua zifuazazo

Juu kabisa ya software nenda katika uwanja umeandikwa tools bofya hapo itakuja menu ina vitu vingi  wewe utachagua create bootable Usb Drive itafunguka box hii hapa 
Wakati huo umechomeka flash yako katika Computer hatua inayo fuata ni ku bofya mahali pameandikwa image source file mahali ulipo save image yako ya window itakuletea window zote zilizo katika mfumo wa image kama hivi



Chagua window unayo taka then Bonyeza Start Button Software itafanya kazi yake mpaka mwisho itakuambia ume fanikiwa sasa una weza ukaweka flash katika computer yoyote na kuweka wendow bila shida.

JINSI YA KUINSTALL WINDOW KATIKA COMPUTER YAKO BAADA YA KUANDAA FLASH.



Weka Flash yako katika computer alafu zima computer yako baada ya hapo washa ,kabla computer haijawaka press button F12 juu kabisa ya computer yako au minya escape 
Baada ya hapo computer itakudai unataka kuboot toka wapi basi chagua mahali pa usb and flash drive uweze ku boot computer yako. Hapo window itafanya installation hadi mwisho kabisa na hatua zingine ni za kawaida tu kuset password pamoja na kuandika user name ya computer.

JINSI YA KUIFANYA FLASH DISK IWE BOOTABLE

Habarini ndugu zetu, leo tunajifunza namna ya kuifanya flash kuwa bootable,

Hii njia mara nyingi hutumika pindi CD-ROM ya computer yako inapokuwa imeharibika, ama computer yako haina CD-ROM, na wakati mwingine ni kwa uharaka wa kufanikisha operating system installations.

Kuna kuweka Bootable kwa ajili ya windows 7/vista ni rahisi zaidi, lakini pia ni tofauti kwa windows xp, na pia nitofauti kwa Ubuntu/linux

http://www.datarecoverybd.com/wp-content/uploads/2015/03/51exav.png

Flash kuwa bootable maana yake ni kuweza kuBOOT computer baada ya BIOS INTERFACE, hii ni kwa ajili ya computer zilizokufa operating systems/ama unapenda kuchange OS 

Hii hapa ni njia rahisi ya kuifanya FLASH kuwa Bootable kwa windows 7/vista
1. Open Command Prompt , hii unaweza kuipata kwa ku bonyeza "start" alafu andika CMD
2. Ikifunguka Andika DISKPART
3. Then ikiisha funguka andika LIST DISK
4. Then Utapata machaguo mbali mbali ya disk zilizopo/zilizokuwa connected kwenye computer
NOTE: disk 0 = internal hard disk
disk1= USB flash
disk2=USB flash or other
Inategemeana na umeconnect flash ngapi
5. Then andika "SELECT DISK 1" kutokana na disk namba ya USB flash yako
6. Then Andika "CLEAN"
7. Then Andika "CREATE PARTITION PRIMARY"
8. Then Andika " ACTIVE"
9. Then Andika "FORMAT FS=FAT32 QUICK"
10. Ikimaliza Andika "EXIT"

SASA BAADA YA HAPO????
Tumia Software yoyote ile kucopy file za operating system hasa windows 7/vista, Ila hapa complex system tuna recommend tumia "POWER ISO" kuextract windows Files (NimeATTACH unaweza ukaidownload.)

http://imag.malavida.com/mvimgbig/download/poweriso-921-1.jpg

FAHAMU JINSI YA KUSET INTERNET KWENYE SIMU YA ANDROID


Ulishawahi kununua simu ukaweka lain lakini ikakataa kusoma data au ulishawahi kurestore simu ikakataa kusoma internet baada ya kuwaka lakini kabla ilikuwa inasoma data tena 3g? sasa ngoja nikwambie kitu
Ili simu za android ziweze kusoma mtandao wa internet ninlazima zifanyiwe setting za kuziwezesha kusoma mtandao wa internet. setting hizo hujulikana kama access point. hivyo kama simu yako haina hizo access point haiwezi kusoma mtandao wa internet hata kama una kifurushi cha internet labda kama hizo access point zitaingia automatic kutoka kwa ISP (INTERNET SERVICE PROVIDER mfano TIGO,VODA, AIRTEL n.k) wako.
hivyo leo nitakuelekeza kutengeneza access point yako ambayo itakuwezesha kutumia internet kwenye simu yako kupitia lain yoyote ambayo utakuwa umejiunga kifurushi.

SASA FATA HATUA HIZI ILI KUTENGENEZA ACCESS POINT KWENYE SIMU YAKO

HATUA YA 1
fungua menu ya simu yako ya android kisha nenda kwenyesetting


HATUA YA 2
   Baada ya hapo nenda palipo andikwa wireless & network, ukisha kuwa hapo bonyeza neno more

HATUA YA 3
 Kisha bonyeza neno MOBILE NETWORKS


HATUA YA 4
Kisha bonyeza  ACCESS POINT NAME



HATUA YA 5
Bonyeza menu ya simu yako ( hii inatofautiana kulingana na simuila utaitambua kwakuwa huwa na alama ya mistari mitatu chini kwa simu yako kulia au kushoto, au huwa imeandiwa kabisa kwa baadhi ya simu au huwa ni vidot vitatu kwa baadhi ya simu juu ya display upande wa kulia au kushoto juu)

boyeza hapo kisha chagua neno New APN.



ikifunguka itakuwa kama hivi 
 







SASA FATA HATUA HIZI TENA
 a. NAME
         kwemye jina andika jina lolote hata la kwako

b. APN  
      kwenye APN  hapo andika  neno "internet"

c.   APN type
       kwenye APN type chagua "default" au kama kiboksi kinataka uandike wewe andika neno "default"

d.  Proxy,port,username,password,server,MMSC,MMS proxy,MMS port
           hivi achana navyo kwani havina umuhimu.

e. Authentication type
        hapo chagua PAP au chagua PAP or CHAP

f.   APN Protocal
       hapo chagua IPV4 au chagua IPV4 or IPV6

g.  Bearer au Data bearer
         chagua "unspecified" 

ukimaliza kujaza hapo bonyeza tena menu ya simu yako kisha bonyeza neno  save, na hapo utakuwa tayari umeshatengeneza access point yako ambayo itakuwezesha kutumia internet kwenye simu yako ya Android.
Sasa rudi mwanzo kabisa wa simu yako kisha nenda sehemu ya kuwezesha data kisha wezesha hiyo data angalia kama itasoma ( itaanza kusoma E na kisha 3G) kama ina sapoti 3G na itasoma E kama haisapoti 3G
 Ili simu yako iweze kushika data vizuri iweke kwenye flight mode kwa muda wa sekunde kumi kisha itoe kwenye flight mode.

Jinsi ya kufanya kama computer yako imeganda (kustack)


Huenda unasumbuliwa na tatizo la kustack la mara kwa mara kwenye computer yako na inakuuma sana na kukufanya ukasirike kwani unashindwa kufanya kazi zako kwa raha. lakini pia hujui nini ufanye ili kuepukana na tatizo hilo. basi nikukaribishe hapa ili uweze kujua nini unatakiwa kufanya

Hizi ni baadhi ya njia za kufuata...

Restart computer yako
Sawa pengine hili linajulikana kwa kiasi kikubwa. Japokuwa wengine wanazani ni kuchomoa waya wa umeme kifaa kikizima wakiwashe tena. Usifanye hivyo jaribu kushikilia kitufe cha kuzima kwa sekunde 5 mpaka 10, bila shaka kifaa chako kitaji ‘Restart’
Kuna mambo mengi yanweza yakajitokeza wakati kompyuta yako inawaka. Kwa leo ngoja tuangalia yale ambayo yanatokeaga san asana.

– Kompyuta Inawaka Bila Tatizo Lolote
Hii inaweza ikawa siku yako, kama kompyuta yako ikiwaka salama kabisa kitu cha kwanza kufanya ni kuhifadhi taarifa zako za muhimu (Back Up). Hii itakuwa ni njia nzuri hasa kama kuna tatizo lingine ambalo lipo njiani, hii itakusaidia sana kuliko kuhangaika kupata taarifa zako katika kompyuta ambayo imekufa.
Baada ya hapo tumia kompyuta yako kama kawaida tuu pengine mpaka itakapo ‘freeze’ tena, japokuwa inaweza isifanye hivyo tena. Kama ikifanya hivyo endelea kusoma njia nyingine

– Kompyuta Inakuuliza Jinsi Ya Kuwaka
Unakuwa una ‘Restart’ kompyuta yako inaweza ikasema kulikuwa na tatizo katika Windows na inaweza ikakuuliza kama unataka kuiwasha katika hali ya kawaida au kwa kutumia njia ya tahadhari ( Normally Au Safe Mode). Kwa mara ya kwanza kabisa chagua Normally na kisha fanya hifadhi (Back Up) ya taarifa zako za muhimu. Kisha tumia kompyuta yako kama kawaida tuu na uangalia kama itaganda tena.
Kwa mara ya pili kama kompyuta yako imeganda chagua kuiwasha kwa njia ya usalama na tahadhari (Safe Mode). Kama ikiwaka basi kompyuta yako inaweza ikawa na tatizo la ‘Software’ au ‘Hardware’. Lakini usikate tama endelea kusoma unaweza ukapata ufumbuzi.

– Kompyuta Imeganda (Ghafla) Tena
Kama kompyuta ikiendela kuganda tena baada ya kutumia njia zote mbili za kuwasha yaani kuwasha kwa njia ya kawaida na kutumia ile njia ya kiusalama (Safe Mode). Bila shaka hapo kompyuta yako inaweza ikawa na tatizo katika ‘Hardware’ au ‘Software’ ingawa mara nyingi linakuaga ni lile tatizo la Hardware.

Ishara Ya Kompyuta Yenye Tatizo

Njia Ya Kukabiliana Na Matatizo Ya Software

Mara nyingine kuganda kwa kompyuta kunaweza kukawa kumesababishwa na programu ambayo haifanyi kazi katika kiwango chake cha ufanisi. Fungua ‘ Task Manager ’ nia rahisi bofya CTRL + SHIFT + ESC ili kuifungua na kisha chagua sehemu ya ‘ Performance ’ kama unatumia Windows 8.1 au 10 itakubidi uki ‘click’ katika eneo la ‘ More Details’ katika upande wa chini wa Task Manager.
Anza kutumia kompyuta yako kama kawaida tuu lakini macho yako yawe katika eneo la CPU, Memory au Disk (ndani ya Task Manager). Kama kompyuta yako itaganda tena na moja kati ya maeneo hayo yana namba kubwa ukilinganisha na mengine basi hilo linaweza likawa ndio jibu lako. Lijue eneo ambalo lina namba kubwa na kisha ‘restart’ kompyuta yako kama kawaida
Mara hii chagua ‘Process’ ndani ya Task Manager. Kwa mpangilio wa CPU, Memory au Disk, chochote ambacho kilikuwa na namba kubwa mwanzoni wakati kompyuta ilipoganda kisha angalia kipi kitakacho tokea juu kabisa wakati kompyuta inaganda. Hii itakuambia ni software ipi inaleta shida. Ukishapata jibu lako unaweza kuamua kuifuta kabisa katika kompyuta yako au ukasasisha (Update)

Njia Ya Kukabiliana Na Matatizo Ya Hardware

Kabla ya kuikimbiza kompyuta yako kwa fundi husika jua kwamba kompyuta ambayo iliganda baada ya kuwasha kwa kutumia njia zote mbili yaani ile ya kawaida na ile ya kiusalama zaidi na ukiwa ushajaribu njia ile ya kukabiliana na hili kwa kuangalia katika software. Kama haya yote yameshindikana, basi tatizo linaweza kuwa katika ‘hard drive’, CPU yako inachemka sana, tatizo kwenye Memory au njia za kusambaza umeme zina matatizo. Lakini pia inawezekana tatizo likawa ni motherboard japokuwa tatizo hili ni mara chache sana.

Mara kwa mara kwa matatizo ya Hardware, kuganda kutaanza kidogo kidogo lakini kutaongezeka kidogo kidogo. Saa nyingine kunajitokeza wakati kompyuta ikiwa inafanya kazi sana lakini sio wakati ukiwa unafanya mambo ya kawaida kawaida.
Kama ukihisi hili limekukuta basi huna budi kumtafuta fundi anaehusika vizuri na maswala ya kompyuta na ukifika kule muulizie Yule wa Hardware. Huyu atakupa ufafanuzi zaidi na kisha atakusaidia katika kuhakikisha kifaa chako kinarekebishwa.
Baada ya kusema hayo nahisi utakuwa umepata mwangaza juu ya kompyuta yako. Naomba nikushauri kuwa mdadisi, dadisi mapema kabla tatizo halijawa kubwa kwani tatizo kubwa inamaanisha gharama kubwa.

Fahamu Code TISA za kujaribu simu yako ya Android kabla ya kuinunua kuepusha usumbufu.


                                                                                                                                                               








Mara nyingi tumekuwa tukinunua simu dukani bila kuijaribu kiukamilifu hivyo baadhi ya matatizo kuyajua bada ya siku kadhaa kupita, na urudishapo simu hiyo waweza pata usumbufu mkubwa sana kutoka kwa mmiliki wa duka, Leo nakupatia CODE ambazo utatumia kujaribu simu mpya dukani bila kuwako na line yeyote ndani ya simu na waweza kujua kama simu hiyo inamatatizo ya kiutendaji au Laa.                                                                                                                                                                                               Code hizo ni -:
  
  1. *#*#4636#*#*  –  Code hii itakupatia maelezo kuhusu simu yako, maelezo kuhusiana na battery na matumizi
  2. *#*#34971539#*#* kuonesha maelezo yote kuhusiana na kamera na ubora wake.
  3. *#*#232339#*#* AU *#*#526#*#* Njia ya kujaribu ufanyaji kazi wa Wireless
  4. *#*#1472365#*#*  – kuangalia uhai wa  GPS
  5. *#*#1575#*#* – Njia mbadala ya kujaribu GPS
  6. *#*#0283#*#* – Jinsi ya kujaribu ‘Packet Loopback’
  7. *#*#0*#*#* – Majaribio ya tach screen yako (LCD display)
  8. *#*#0673#*#* AU *#*#0289#*#*  – Majaribio ya sauti
  9. *#*#0842#*#* – Majaribio ya sauti mtetemo (Vibration) na Mwito wa muwako (Backlight)

JIFUNZE JINSI YA KU UPDATE SIMU YAKO YA ANDROID


Kama unatumia simu ya Android basi kuna uwezekano wa wewe kufanya kitu kinachoitwa update.  hii itakusaidia wewe kuweza kupata vitu vipya ambavyo vinatakiwa kuingia kwenye simu yako yaani new android features. 
 Wakati mwingine kupitia ku update simu yako ya android kunaweza kukusaidia wewe kupata operating system mpya ambayo itakuwa imeachiwa na google katika kipindi hicho. mfano kama unatumia Android version ya 4.0 basi kupitia update unaweza ukapata mpya yaani Android version ya 4.4 au hata ya 5.0
    ili uweze kufanya update ya simu yako ya Amdroid unapaswa kufanya yafuatayo.

hakikisha simu yako ina internet ya kutosha au upo kwenye wi-fi yenye nguvu
hakikisha umefanya back up ya Data zako zote.
Ili ku back up data zako  ingia kwenye setting kisha nenda kwenye sehemu iliyoandikwa backup & restore


settings icon

kisha weka tiki palipo andikwa backup data.

  baada ya hapo fata hatua hizi tena

Nenda kwenye simu yako ya android kisha ingia kwenye setting




kisha nenda palipo andikwa about phone. 

about phone icon

kabla ya kuendelea hakikisha unaangalia ni aina gani ya software system ya simu yako unatumia. nenda hapa

android version

baada ya hapo nenda sehemu palipo andikwa system update/software update. kisha bonyeza hapo
Image titled Update an Android Step 4

kisha nenda palipo andikwa  check now

Image titled Update an Android Step 5

kama nilivyokwambia awali ili kuweza kupata update ya simu yako lazima uwe na kifurushi cha internet au uwe kwenye wi-fi
kama kuna UPDATE basi itakuja na itataka uidownload weka yes. 
ikimaliza kudownload  itakuletea option ikikwambia INSTALL/RESTART bonyeza hapo


Image titled Update an Android Step 6

simu itajizima na kujiwasha. subiri imalize usiizime kwani inaweza kushindwa kumaliza na hivyo ukaaribu simu yako. ili kuhakikisha simu haizimiki kwa kukosa chaji chomeka simu yako kwenye chaji wakati inafanya installation ya hizo update
ikimaliza simuitajizima na kujiwasha yenyewe.
NJIA HIZI ZINAWEZA TUMIKA HATA KWA ANDROID TABLETS
ANGALIZO
kama ikiwaka alafu ikawa ina stack basi unatakiwa kui reboot simu yako ili kuiweka sawa